Picha ya uwanja utakaojengwa kutumika wakati wa michuano ya 2022 Mwenyekiti wa shirikisho la kandanda ulimwenguni, FIFA, Sepp Blatter, amesisitiza ilikuwa kosa kuchagua Quatar kuwa mwenyeji wa kombe la dunia la mwaka wa 2022. Katika mahojiano na televisheni nchini Uswizi, Sepp Blatter aliulizwa iwapo kuiruhusu Quatar kuwa mwenyeji wa kombe hilo ambalo huchezwa kati ya mwezi Juni na Julai ilikuwa kosa, hasa ikizingatiwa kuwa hali ya hewa katika nchi hiyo hufikia hadi nyuzijoto 50 wakati huo. Alijibu kwa kukiri na kuongeza kuwa kila mtu hukosea maishani. Alipinga madai kwamba taifa hilo lilikuwa limelipia michezo hiyo. Aliongeza kuwa kamati inayojumuisha maafisa wa FIFA walikuwa wamedhibitisha uwezekano wa taifa hilo kuwa mwenyeji ijapokuwa walikuwa wamepokea taarifa kuhusu vipimo vya juu vya jot.



MOHAMED MATUMLA AMGALAGAZA NASSIBU RAMADHANI KWA POINT NA KUIBUKA NA PIKIPIKI



Bondia Mohamed Matumla kushoto akimwadhibu Nassibu Ramadhani wakati wa mpambano wao wa raundi kumi uliofanyika siku ya sikukuu ya krismas na kugombania pikipiki yenye thamani ya shilingi milioni 1.9 Matumla alishinda kwa pointi mpambano huo na kuibuka na bodaboda picha na
Bondia Mohamed Matumla kushoto akipambana na Nassibu Ramadhani wakati wa mpambano wao  uliofanyika siku ya sikukuu ya krismas na kugombania pikipiki yenye thamani ya shilingi milioni 1.9 Matumla alishinda kwa pointi mpambano huo na kuibuka na bodaboda picha na
Bondia Lulu Kayage kushoto akipambana na Mariam Abdallah wakati wa mpambano wao wa kusherehekea sikukuu ya krismas kayage alishinda kwa k,o picha na


lulu akinyooshwa mkono juu baada ya kushinda


l
Bondia Lulu Kayage kushoto akipambana na Mariam Abdallah wakati wa mpambano wao wa kusherehekea sikukuu ya krismas kayage alishinda kwa k,o picha n
Bondia Hamis Ajari kushoto akipambana na Cosmas Cheka wakati wa mpambano wao uriofanyika wakati wa sikukuu ya krismas cheka alishinda kwa point pic


Bondia Sadiq Abdulazizi kushoto akipambana na Juma Fundi wakati wa mpambano wao uliofanyika wakati wa sikukuu ya krismas juma fundi alishinda kwa point mpambano uho picha na
Baadhi ya mashabiki waliouhulia mpambano huo uliokuwa mkali na kutoa burudani ya aina yake kwa mashabiki nchini



 

Search This Blog

Wednesday, December 25, 2013

MOHAMED MATUMLA AMGALAGAZA NASSIBU RAMADHANI KWA POINT NA KUIBUKA NA PIKIPIKI



Bondia Mohamed Matumla kushoto akimwadhibu Nassibu Ramadhani wakati wa mpambano wao wa raundi kumi uliofanyika siku ya sikukuu ya krismas na kugombania pikipiki yenye thamani ya shilingi milioni 1.9 Matumla alishinda kwa pointi mpambano huo na kuibuka na bodaboda picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com
Bondia Mohamed Matumla kushoto akipambana na Nassibu Ramadhani wakati wa mpambano wao  uliofanyika siku ya sikukuu ya krismas na kugombania pikipiki yenye thamani ya shilingi milioni 1.9 Matumla alishinda kwa pointi mpambano huo na kuibuka na bodaboda picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com
Bondia Lulu Kayage kushoto akipambana na Mariam Abdallah wakati wa mpambano wao wa kusherehekea sikukuu ya krismas kayage alishinda kwa k,o picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com


lulu akinyooshwa mkono juu baada ya kushinda


l
Bondia Lulu Kayage kushoto akipambana na Mariam Abdallah wakati wa mpambano wao wa kusherehekea sikukuu ya krismas kayage alishinda kwa k,o picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com
Bondia Hamis Ajari kushoto akipambana na Cosmas Cheka wakati wa mpambano wao uriofanyika wakati wa sikukuu ya krismas cheka alishinda kwa point picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com


Bondia Sadiq Abdulazizi kushoto akipambana na Juma Fundi wakati wa mpambano wao uliofanyika wakati wa sikukuu ya krismas juma fundi alishinda kwa point mpambano uho picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com
Baadhi ya mashabiki waliouhulia mpambano huo uliokuwa mkali na kutoa burudani ya aina yake kwa mashabiki nchini

MISS TANZANIA 2013 ASHEREHEKEA SIKUKUU YA X - MASS PAMOJA NA WATOTO YATIMA MOROGORO



 Miss Tanzania 2013 Happiness Watimanywa Akikabidhi zawadi waliotoa katika kituo hicho kwa Mama Mkuu wa Wa shirika la Masista wa Moyo safi wa Maria Sista Flora Chuma..
 Miss Tanzania 2013 Happiness Watimanywa (pichani), Leo amejumuika na watoto yatima wa kituo cha Mgolole  kilichopo Bigwa nje kidogo ya Mji wa Morogoro. Mrembo huo ameungana na warembo wengine wawili , akiwemo Miss Kanda ya Mashariki Missa Clara Pamoja  Sabra Islam Miss Morogoro 2013 . Miss Tanzania 2013 Happiness Watimanywa.Aliongozana na Wazazi wake pamoja na Ndugu jamaa na marafiki zake  
 Mkurugenzi wa  kamati ya Miss Tanzania Hashim Lundega Akiwa na  Katibu wa Miss Tanzania Bosco Majaliwa leo awlipoongozana na Miss Tanzania 2013 Happiness Watimanywa Alipotembelea Kituo cha Kulea watoto Yatima cha Mgolole Kinachomilikiwa na Masista wa Moyo safi Wa Maria  Cha Mkoani morogoro
 Watoto wa kituo cha kulea watoto yatima cha masista wa Moyo Mtakatifu wa Maria cha Mgolele mkoani Morogoro wakiwa katika Picha ya Pamoja leo walipopata Ugeni Kutoka kwa Miss tanzania Happiness Watimanywa Aliyeambatana na wakurugenzi wa Miss tanzania Pamoja na Wazazi wake ndugu na jamaa wake wa Karibu.
 Ndugu na Marafiki wa  Miss tanzania 2013 waliomsindikaza Happiness Watimanywa  Alipotembelea kituo cha watoto yatima cha mjini Morogoro..

JAMES KISAKA AFARIKI DUNIA, MUNGU AILAZE ROHO YA MAREHEMU MAHALA PEMA PEPONI AMINA.

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limepokea kwa masikitiko kifo cha aliyekuwa kocha wa makipa wa Simba, James Kisaka (57) kilichotokea leo asubuhi (Desemba 25 mwaka huu) katika Hospitali ya Burhani, Dar es Salaam.
Msiba huo ni mkubwa katika familia ya mpira wa miguu kwani Kisaka kabla ya kuwa kocha alikuwa mchezaji katika nafasi ya kipa. Mbali ya Simba, timu nyingine alizowahi kudakia ni Ndovu ya Arusha, Volcano ya Kenya na Small Simba ya Zanzibar.
Akiwa mwanafunzi Shule ya Sekondari Tambaza jijini Dar es Salaam aliwahi kuchezea timu za Oysterbay Stars, Eleven Stars ya Msasani, Sigara wakati ikicheza Ligi ya Temeke na Nyota Nyekundu kabla ya kutua Simba.
Pia alikuwemo kwenye timu ya Taifa ya vijana iliyokwenda Zimbabwe kwenye sherehe za uhuru wan chi hiyo mwaka 1980. Vilevile alikuwa mmoja wa wachezaji waliounda kombaini ya Tanzania ya UMISSETA akiwa na akina Said George, Nico Njohole, George Kulagwa na wengine. Hivyo mchango wake katika mchezo huu tutaukumbuka daima.
Kwa mujibu wa kaka wa marehemu, Benny Kisaka, James alikuwa akisumbuliwa na ugonjwa wa miguu kufa ganzi na matatizo ya kutoona vizuri.
Msiba uko nyumbani kwake Mbezi Mwisho (Kwa Yusuf), na anatarajia kuzikwa nyumbani kwao Kijiji cha Lusanga, Muheza mkoani Tanga.
TFF tunatoa pole kwa familia ya marehemu Kisaka, klabu ya Simba na Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) na kuwataka kuwa na subira na uvumilivu katika kipindi hiki kigumu cha msiba huo mzito.
Marehemu Kisaka ameacha mjane na watoto wanne. Bwana alitoa, Bwana ametwaa. Jina lake lihimidiwe.
Boniface Wambura Mgoyo
Kaimu Katibu Mkuu
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)

Tuesday, December 24, 2013

MOHAMED MATUMLA NASIBU RAMADHANI KUMARIZA UBISHA CHRXMAS


Bondia Mohamed Matumla kushoto na Nassibu Ramadhani wakitunishiana misuli baada ya kupima uzito kwa ajili ya mpambano wao leo katika

ukumbi wa friends corner hotel manzese Dar es salaam leo katikati ni promota wa mpambano huo kaike siraju Picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com


Promota kaike Siraju akiwainua juu mikono Bondia Mohamed Matumla kushoto na Nassibu Ramadhani kwa ajili ya mpambano wao wa kugombea pikipiki siku ya sikukuu ya Xmasi Picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com

MTAWALA NA MWESIGA WAPATA MASHAVU TFF.




DAUDA TV: KAMA HUKUBAHATIKA KUYAONA MABAO YA MCHEZO WA SIMBA NA YANGA ( NANI MTANI JEMBE ) HAYA HAPA!

MWAKALEBELA AKANUSHA KUKOSA KIBARUA CHA UKATIBU MKUU TFF - ASISITIZA YUPO TAYARI KUFANYA KAZI NYNGINE NA TFF SIO UKATIBU


MCHEZAJI WA BORA WA LIGI YA BRAZIL - EVERTON RIBEIRO ASEMA ATAICHAGUA MAN UNITED MBELE YA REAL MADRID

Kiungo wa kibrazil Everton Ribeiro kwa mara nyingine ameelezea matamanio ya kujiunga na klabu ya Manchester United. 

United iliwatuma maskauti wake wa vipaji kwenda nchini Brazil kumuangalia staa huyo wa timu ya Cruzeiro na kocha David Moyes anafikiria kutuma ofa rasmi ya £12million ili kukamilisha usajili wa kiungo huyo, ambaye mwezi uliopita alishinda tuzo ya kuwa mwanasoka bora wa ligi ya Brazil.

Hata hiyo, United watakabiliana na upinzani kutka kwa Liverpool na Real Madrid ambao nao wamevutiwa na mchezaji huyo.

Ribeiro ambaye huko nyuma aliwahi kucheza katika mashindano ya vijana na United alipoulizwa na Globoesporte kama angependelea kujiunga na United badala ya Madrid, kiungo huyo mwenye miaka 24 alisema: ‘Ndio, ningependea kucheza United, mfumo ambao United wanaendesha timu ni bora kabisa duniani. Nimewahi kuwepo mahala pale na pia nilienda kupata mafunzo kutoka Alex Ferguson nilipokuwa kinda. ’

Wakala wa mchezaji huyo Robson Ferreira hivi karibuni alinukuliwa akisema: Manchester United wanamtaka Ribeiro,  David Moyes amevutiwa sana. Nilishaenda England na nikaongea rasmi na United.’

FALCAO: RONALDO NI MCHEZAJI BORA ZAIDI YA LIONEL MESSI

Mshambuliaji wa Monaco  Radamel Falcao anaamini kwamba mshambuliaji wa Real Madrid  Cristiano Ronaldo ni mchezaji mzuri kuliko staa wa klabu ya Barcelona Lionel Messi.

Mchezaji huyo wa Colombia anawakubali wachezaji wote wawili, ingawa Falcao anaamini Cristiano ni bora zaidi ya Messi.

"Messi na Cristiano ni wachezaji muhimu na wakubwa duniani leo hii lakini, kwangu mimi naamini Ronaldo ni bora zaidi," alisema mchezaji huyo mwenye miaka 27 alipoongea na El Tiempo.

Falcao pia amesema ni Cristiano Ronaldo anayestahili kuwa mchezaji bora wa dunia katika tuzo za Ballon D'or zitakazotolewa mwezi ujao ambapo Ronaldo anapambana na Ribery pamoja na Messi.

EDIBILY LUNYAMILA APATA NAFUU,

Hali ya winga wa zamani Edibily Lunyamila inaendelea vizuri,leo hii asubuhi mwandishi amepita kwenye hospitali ya Mwananyamala na kukuta Jopo la madaktari saba akiwemo Daktari bingwa wa tiba za michezo,Dr Mwankemwa wakimshughulikia vizuri mgonjwa huyo.

Pia leo asubuhi wachezaji kadhaa wa zamani kama vile Silvatus Ibrahim,Mohamed Hussein na Vincet Peter walipita kumjulia hali mwenzao,Hapo jana uongozi wa Klabu ya YANGA ulifika hospitalini pale ukiongozwa na Mwenyekiti wa kamati ya mashindano Abdallah Bin Kleb,Nahodha wa zamani Ally Mayai na walipanga asubuhi ya leo wamwamishie kwenye hospitali ya Muhimbili,aliyepewa jukumu hilo alikuwa ni mjumbe wa kamati ya utendaji ndugu Mohammed Binda.

'' Jana viongozi wa Yanga tulikubaliana leo tumwamishie hospitali ya Muhimbili lakini tulipofika leo asubuhi madaktari wa hospitali ya Mwananyamala walitusihi tumwache kwanza kwani walikuwa tayari wanamshughulikia,kutokana na huduma nzuri aliyokuwa anapewa na madaktari wa hapa tumeonelea tumwache kwanza'' alinukuliwa Binda akielezea hali ya mgonjwa.


KATIBU MKUU WA SIMBA AACHIA NGAZI AULA TFF - MWESIGA WA YANGA NAE KUMRITHI ANGETILE


KAMATI ya Utendaji ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) imekutana wikiendi iliyopita na kufikia uamuzi wa kuwapa ajira aliyekuwa katibu wa Yanga, Selestine Mwesigwa na wa Simba, Evodius Mtawala.

Mwesigwa atafanya kazi hiyo chini ya uangalizi kwa kipindi cha miezi sita na endapo TFF atamudu nafasi hiyo atapewa muda zaidi, lakini kama atashindwa basi ajira yake itasitishwa mara moja.

Wakati Mwesigwa akiinasa ajira hiyo aliyoshindania vikali na Michael Wambura, mwenzake wa Simba, Mtawala ameula kwenye Mkurugenzi wa Sheria na Masuala ya Utawala ambayo ni nafasi mpya katika shirikisho hilo.

Kufuatia uteuzi huo ni wazi Mtawala atalazimika kuachia ngazi katika nafasi yake ya ukatibu kwenye klabu ya Simba, huku taarifa zilizoifikia Mwanaspoti usiku wa jana Jumatatu, Mtawala ameihakikishia TFF kwamba tayari ameshawasilisha barua yake ya kuacha kazi kwenye klabu ya Simba.

Mwesigwa na Mtawala watatangwa rasmi leo Jumanne na Rais wa TFF, Jamal Malinzi.

DAUDA TV: EXCLUSIVE INTERVIEW YA MH ZITTO KABWE JUU YA MUSTAKABALI WA SOKA LA BONGO.

Monday, December 23, 2013

HII NDIO TAARIFA RASMI YA KUFUKUZWA KOCHA WA YANGA ERNST BRANDTS



Uongozi wa klabu ya Young Africans SC umempatia taarifa (Notice) ya siku ya thelathini (30) kocha mkuu mholanzi Ernie Brandts juu ya kusitisha mkataba wake kuanzia jana Disemba 22 mwaka huu.
Maamuzi hayo yanafuatia muenendo wa matokeo mabaya katika michezo iliyopita ya Ligi Kuu, kirafiki na bonanza la Nani Mtani Jembe dhidi ya Simba SC mwishoni mwa wiki.
Hatua ya Young Africans SC kusitisha huduma na Brandts isichukuliwe kama chuki bali ni moja ya sehemu ya kuhakikisha tunaboresha benchi la ufundi ili tuweze kupata matokeo mazuri katika Mashindano yanayotukabili.
Ukitazama uwezo wa mchezaji mmoja mmoja wa Yanga SC na wapinzani wetu, na soka tulilocheza kwenye mchezo wa mwishoni mwa wiki kwa kweli ni dhahiri mwalimu amefikia mwisho kimbinu na hana njia mbadala.
Young Africans SC imekua ikicheza chini ya kiwango katika michezo ya Ligi Kuu hali iliyoplekea kupata ushindi kwa tabu na wakati mwingine timu kupoteza pointi.
Kufuatia kupewa taarifa ya siku 30, Brandts ataamua mwenyewe kama ataendelea kusimamia mazoezi ya timu au kuondoka moja kwa moja kabla ya muda huo ukiwa haujakamilika.
Ikiwa Brandts ataondoka mapema timu itaendelea na mazoezi kama kawaida katika kila siku asubuhi katika uwanja wa bora kijitonyama kujiandaa na mzunguko wa pili wa Ligi Kuu na mashindano ya kimataifa chini ya kocha msaidizi Fred Felix “Minziro”.
Ili kuhakikisha timu inafanya vizuri katika mzunguko wa pili wa Ligi Kuu ya Vodacom na mashindano ya kimataifa uongozi unakamilisha maandalizi ya safari ya kambi nje ya nchi na taratibu zote zitakapokamilika tutawajulisha.
Aidha uongozi upo katika mchakato wa kumapata mrithi wa Brandts ambaye ataungana na timu kwa ajili ya maandalizi ya mzunguko wa pili na Mashindano ya klabu Bingwa Afrika.
Mwisho tunawaomba wanachama, wapenzi na washabiki wa Yanga wasivunjike moyo kufuatia matokeo ya bonanza mwishoni mwa wiki, uongozi unajipanga kuhakikisha timu inaimarika kwenye benchi la ufundi na kurudisha furaha katika mzunguko wa pili wa VPL.


Abdallah Bin Kleb
Mwenyekiti - Kamati ya Mashindano
Young Africans Sports Club.



DAR ES SALAAM
23 Disemba, 2013

BREAKING NEWS…..! HALI NI MBAYA…! LUNYAMILA ANAPUMULIA MASHINE HOSPITALI YA MWANANYAMALA.


WINGA wa zamani wa Yanga na Taifa Stars, Edibily Lunyamila leo hii asubuhi amekimbizwa katika hospitali ya Mwananyamala baada ya kusumbuliwa na kifua na sasa anapumua kwa msaada wa mashine.

Mtandao huu ulifanikiwa kufika hospitalini hapo muda mfupi baada ya winga huyo kukimbizwa hospitalini hapo baada ya kuzidiwa tangu jana usiku akiwa nyumbani kwake Mbezi jijini Dar es Salaam.

Shaffihdauda.com imemshuhudia Lunyamila akiwa amelala kitandani katika wodi ya wanaume namba namba 5 kitanda namba 16 katika hospitali hiyo ya rufaa ya Kinondoni.





Daktari Madirisha Pascal anayemuhudumia winga huyo wa zamani, Lunyamila anasumbuliwa na tatizo la kifua ambalo linamfanya ashindwe kupumua vizuri.

“Kama mnavyomuona anapumua kwa msaada wa mashine na bado tunaendelea kumfanyia uchunguzi ili kubaini nini kinachomsumbua zaidi,” alisema Pascal.

Mmoja wa ndugu wa Lunyamila, Lameck John alisema kwamba, mchezaji huyo wa zamani alianza kujisikia vibaya jana Jumapili na leo asubuhi hali yake ilibadilika ndipo walipomkimbiza hospitali.




 Lunyamila alivyokuwa enzi anaichezea Yanga..



 

“Alianza kulalamika hawezi kupumua na kifua kinamsumbua pia mbavu zilikuwa zikimuuma, baada ya majibu ya vipimo tutajua kinachomsumbua zaidi,” alisema Lameck.

Kutokana na hali iliyoonekana hospitalini hapo, Lunyamila anahitaji huduma ya haraka ili kuweza kuokoa uhai wake kwani anapumulia mashine akiwa katika sehemu yenye joto kali hivyo anapambana na vitu vingi kwa wakati mmoja...

Taarifa za kiuchunguzi zilizofanywa na mwandishi wetu zimebaini Lunyamila anasumbuliwa na ugonjwa wa moyo.
''Nilikuja jana hospitali ya mwananyaala ikagundulika moyo wangu umekuwa mkubwa,hivi sasa naenda muhimbili kwa ajili ya vipimo zaidi nikifika na kukutana na daktari nitakujulisha ''
ilipofika mchana wa leo mwandishi alipokea simu kutoka kwa Lunyamila akimwambia ameambiwa arejee tena hospitali ya Mwananyamala.

KASEBA AMCHAKAZA ALIBABA KWA K,O RAUNDI YA 4


Bondia Japhert Kaseba kushoto akioneshana umwamba wa kutupiana makonde na Alibaba Ramadhani wakati wa kugombania ubingwa wa Taifa uliofanyika Manzese Dar es salaam Kaseba alishinda kwa KO ya raundi ya nne ya mpambano huo Picha na superdboxingcoach.blogspot.com
Kanda kabongo akimuhuumia Japhert Kaseba
Bondia Omari Nampekecha 'peche boy' kushoto akipambana na hasani Kiware wakati wa mpambano huo nampekecha alishinda kwa pointi picha na superdboxingcoach.blogspot.com
Kaseba akiwa na familia yake pamoja na mashabiki baada ya kushinda mchezo wake
Bondia Pendo Njau kushoto akiwa na bondia Llulu Kayage wakati wa mpambano huo
mashabiki wakiangalia mpambano
Wapiganaji wa mpambano wa Kick Boxing kareem kutch kushoto akipambana na Hassani Juma 'Tata Boy' wakati wa mpambano huo kutch alishinda kwa point picha na superdboxingcoach.blogspot.com
Wapiganaji wa mpambano wa Kick Boxing kareem kutch kushoto akipambana na Hassani Juma 'Tata Boy' wakati wa mpambano huo kutch alishinda kwa point picha na superdboxingcoach.blogspot.com

YANGA YAMTIMUA KOCHA WAKE ERNEST BRANDTS

MUDA mfupi uliopita klabu ya soka ya Yanga imetangaza kusitisha mkataba na kocha wake Ernest Brandts baada ya kutoridhishwa na mwenendo wa timu hiyo.

Kwa mujibu wa Ofisa Habari wa Yanga, Baraka Kizuguto, mkataba wa Brandts ambaye ni raia wa Uholanzi umesitishwa rasmi leo hii asubuhi na ameshakabidhiwa barua ya kumtaarifu juu ya hali hiyo.

“Tumesitisha mkataba na kocha wetu na ameshakabidhiwa barua yake, huo ni uamuzi wa uongozi mzima wa Yanga, kila kitu kimeenda sawa katika kuachana naye,” alisema Kizuguto.

Tetesi za Brandts kutimuliwa zilizagaa jijini Dar es Salaam tangu jana muda mfupi baada ya Mwenyekiti wa Yanga, Yussuf Manji kwamba hata kama klabu itaamua kuachana na kocha huyo itafuata taratibu zote.

Uamuzi huo wa Yanga unaonekana pia kuchagizwa zaidi na kipigo cha mabao 3-1 dhidi ya Simba katika mchezo maalum wa kirafiki maarufu kama Nani Mtani Jembe uliochezwa wikiendi iliyopita Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

BREAKING NEWS: TRESOR MPUTU AIHAMA RASMI TP MAZEMBE


Sunday, December 22, 2013

DAUDA TV: CLOUDS MEDIA ILIPOWATANDIKA MASHABIKI WA YANGA MABA0 3-2.

Hapo siku ya Ijumaa mwishoni mwa juma hili CLOUDS MEDIA GROUP 'The Dream Team'' ilipambana na mashabiki wa YANGA waliopo kwenye mitandao ya kijamii, baada ya dakika 90 za mchezo huo uliopigwa kwenye dimba la Tanganyika Packers, CLOUDS waliibuka na ushindi wa mabao 3-2 yaliyofungwa na James Tupatupa,Shaffih Dauda na Said Tully.


BAO LA YANGA... 

BAO LA KWANZA LA CLOUDS LILILOFUNGWA NA TUPATUPA. 
BAO LA PILI LA CLOUDS LILILOFUNGWA NA DAUDA. BAO LA TATU LA TULLY

SIMBA NDIYO MTANI JEMBE

Na Baraka Mbolembole

Yanga, mechi yake ya jumamosi katika uwanja wa Taifa, ilimalizika kwa
mlinzi wake wa kati, Kelvin Yondan kuoneshwa kadi nyekundu baada ya
kufanya kosa la kumvuta jezi, kiungo-mshambuliaji, Ramadhani Singano
na kupelekea kupata kadi ya pili ya manjano dakika kumi kabla ya
kumalizika kwa mchezo.

Kocha wao, Ernie Brandts aliamua kufanya mabadiliko ya wachezaji
watatu kwa mpigo, baada ya kuwaingiza uwanjani, Saimon Msuva, Emmanuel Okwi, na Said Dilunga katika dakika ya 46. Zote hizo zilikuwa dalili za presha, na hakika kuwa nyuma kwa mabao 2-0 ndani ya dakika 45
haikuwa ishara nzuri. Yanga waliingia uwanjani wakiwa na hali ya kujiamini, ila mabao y Tamwe yaliondoa hali hiyo na kuzalisha mvurugano kwao.






AMIS TAMBWE
Alifunga bao lake la kwanza baada ya kumalizia kazi nzuri iliyokuwa
imefanywa na Jonas Mkude. Henrry Joseph, Said Ndemla na Harouna
Chanongo, ambao walipigiana pasi za uhakika na kutengeneza nafasi kwa
mshambuliaji huyo aliyekuwa ndani ya boksi. Akamuadaa, Nadir Haroub na
kumalizia vizuri mpira aliopasiwa, na baada ya goli hilo, Simba
wakaonekana kucheza kwa kujiamini na mipango mizuri kuliko Yanga.





Tambwe ambaye alianza pamoja na Awadh Juma katika safu ya
mashambulizi, alifunga tena bao la pili kwa mkwaju wa penati, baada ya
Singano kuangushwa katika eneo la hatari na mlinzi wa kushoto wa
Yanga, David Luhende katika dakika ya 42. Baada ya mabao hayo Simba
ilikuwa bora zaidi ya Yanga kwa muda wote wa mchezo. Mabao ya Tambwe yaliivuruga Yanga, ambao walionekana kurushiana maneno ya lawama kwa wachezaji wao wa safu ya ulinzi. Simba walijiamini zaidi na Jonas Mkude akawa anaichezesha timu na kuwalinda walinzi wake.
       
LOGARUSIC NA UJANJA WA 'SUB'
 Kocha wa timu ya Simba, Logarusic alikuwa na mbinu, pamoja na 'timming' kali kuliko, Ernie Brandts wa timu ya Yanga. Aliamua kumtoa
Said Ndemla na kumuingiza uwanjani, Ramadhani Singano katika dakika ya 26 tu ya mchezo, baada ya kiungo huyo chipukizi kuzidiwa na mchezo.
Dakika sita, baadae akafanya mabadiliko mengine kwa kumpumzisha
kiungo, Henry Joseph ambaye alionekana kupoteza mipira mingi ya hatari
katika eneo lao la ulinzi, na kuonekana akicheza faulo za mara kwa
mara, na Ramadhani Chombo akaingia. Simba, ikabadilika na kucheza
mchezo wa pasi za uhakika huku suala la kumiliki mpira likiwa juu
kuliko kwa upande wa wachezaji wa Yanga.
        YANGA....
Waliingia na timu ileile iliyocheza mara ya mwisho na Simba
katika mchezo wa ligi kuu, oktoba 20, ukimtoa golikipa Juma Kaseja,
ambaye aliingia mahala kwa Ally Mustapha. Walionekana kujiamini zaidi.
Kabla ya mchezo huo walikuwa wamecheza michezo mitatu mfululizo na
mahasimu wao pasipo kufungwa. Athumani Idd ' Chuji', alikuwa na tatizo
kama alilokuwa nalo, Joseph kwa upande wa Simba, alipiga pasi za
hovyo. Hakuonekana sana, na wala hakuwa na haja ya kufanya hivyo.
Alicheza chini ya kiwango chake cha kawaida, na akashindwa kujibadili
mwenyewe na kubadili stahili yake ya upigaji pasi ndefu za juu.
Alijitahidi kuisogeza timu kutoka nyuma na tofauti na Joseph, Chuji aliwasa





sana katika ukabaji. Alikuwa na siku mbaya, kwa kuwa hakupata msaada
wa kutosha kutoka kwa Mrisho Ngassa, ambaye aliamua kujificha pembeni
ya uwanja muda wote..

Simba, iliwaanzisha, Ndemla, Joseph, Jonas Mkude na Haroun Chanongo
katika nafasi ya kiungo, huku Awadh Juma akicheza nyuma kidogo ya
Tambwe. Viungo watatu kati yao wote ni wazuri katika ukabaji, Ndemla,
Joseph na Mkude. Wakati, Chuji akijibidiisha kadri awezavyo, Frank
Domayo, akawa mkimya sana uwanjani, alifanya kazi ya ' kupatrol' mbele
ya Chuji, na kusaidia safu ya ulinzi. Aliogopa kusonga mbele hata
wakati alipotakiwa kufanya hivyo, hakuwa katika kiwango kizuri sana
hasa baada ya eneo la katikati ya uwanja ' kutekwa' na viungo wa Simba.

ULIMUONA KIUNGO HUYU...

Bila shaka, ulimuona. Mkude alionekana kupiga pasi za uhakika '
mwanzo-mwisho', alijimiliki mwenyewe na baadae akaumiliki mchezo na
kuwa kiongozi wa timu yake uwanjani. Alianzisha pasi nzuri katika '
move' ya bao la kwanza, na angeweza kufunga bao kali la kiki ya umbali
mrefu, pale alipouwahi mpira wa rebound. Wakati, Ndemla na Joseph
walipopoteza ' njaa ya mchezo', yeye alijitahidi kuwaweka sawa, kwa
kuwavuruga viungo wa Yanga kwa mchezo wake wa nguvu na akili,
alipokuja kuingia, Singano na baadae, Chombo akaamua kusonga mbele
zaidi na kupiga pasi za kukimbiza, safu ya ulinzi ya Yanga ikawa
inapitika, na baadae, David Luhende akajikuta akiishiwa mbinu na kusababisha penati, endelea kusoma utagundua kwa nini.


HAKUNA SIRI ITAKAYOACHWA IPOTEE
Bao la tatu la Simba, lilikuwa ni goli la kufedhehesha sana,
liliwaumiza wengi kutokana na namna lilivyoandaliwa na kufungwa na
kiungo, Awadh Juma. Ni makosa ya wazi ya golika Kaseja, ambae
alishindwa kufanya maamuzi ya kuuondoa mpira uliokuwa ndani ya uwezo.
Wakati, fulani, Juma aliwahi kushiriki katika maandalizi ya bao kama
lile wakati akiwa kipa wa Simba, msimu uliopita katika mchezo
waliopeteza mbele ya Mtibwa Sugar. Kuna wakati, Juma huwa anaruhusu
magoli ya kipuuzi na alifanya tena hivyo, siku ya jumamosi na
kuigharimu timu yake. Huwa anajiamini kupita kiasi, jambo ambalo
wakati mwingine linapelekea wapenzi wa soka kumuona ni mtu mbaya
Wazee wa klabu ya Yanga wanasema ' walijua kuwa Juma amekuja kuwafungisha', je anaweza kuzungumza kitu baada ya tukio la kuwazawadia Simba bao la tatu?. Brandts aliamua kumpa adhabu kali, ya kutomfanyia mabadiliko hadi mwisho. Yanga, wakome sasa kusajili hovyo wachezaji wa Simba.
Kelvin Yondan alionekana kuwa mpambanaji sana, japo baadae akajikuta
akiadhibiwa na kuondoshwa mchezoni. Alikuwa imara yeye binafsi, jambo
ambalo liliongeza unafuu katika ngome yao. Alionekana kutuliza kichwa
chake, ila baada ya kufungwa bao la kwanza akaonekana kuwa ' mapepe'
kama patna wake, Nadir Haroub. Alionekana kuchukizwa na kitendo cha
Tambwe kufunga bao rahisi mbele ya nahodha, Nadir, na kuanza kucheza
kwa ' kisirani'. Walicheza pamoja kwa mara nyingine na ndani ya miezi
miwili wamejikuta wakiruhusu kufungwa magoli matano na mahasimu wao.
Mahusiano yao yamekuwa mabaya tangu, oktoba, na kitendo cha kuamua
kumfokea mwenzake huyo, ni ishara kuwa hawaaminiani tena. Nadir na mahusiano yao ya kiuchezaji yameshindwa kuwa mazuri.

 JOSEPH OWINO, DONALD MUSOTI
Siku nyingine tena ya kujaribu kila kitu, na mwishowe kukosa matokeo
bora. Didier Kavumbagu na Hamis Kiza walitumia muda mwingi wa dakika
45 walizokuwepo uwanjani katika ' mifuko' ya Owino na Musoti, na Okwi
aliyeingia dakika ya 46 alitumia robo saa ya kwanza kuzunguka uwanjani
akitafuta mpira wa kugusa. Walinzi hao wa kati wa Simba, walicheza
mchezo wa kutotanuka hovyo ili kuhakikisha washambulaji hao hawaleti
madhara kwa kipa, Ivo Mapunda. Wakati safu ya ulinzi ya Yanga,
ikiandaa mazingira ya kufungwa, kwa upande wa Simba walikuwa imara na
hawakuruhusu kufanya makosa yasiyo na ulazima. Waliziba mianya ya
viungo wa Yanga kuwapasia pasi, na wakawa katikati mbele ya kipa wao.
 NADIR HAROUB ' CANNAVARRO'
Alikuwa mchezaji mzoefu zaidi uwanjani kwa upande wa Yanga, na katika
umri wa miaka yake 31 sasa, alitakiwa kuwa mtulivu na kiongozi wa
wenzake uwanjani, Nahodha huyo wa Yanga, hakuwa mtulivu na kumtuliza
Tambwe hasifunge mbele yake, alimruhusu mshambuliaji huyo kumuweka nje ya eneo lake na kufunga goli rahisi. Alishindwa kumtawala kwa kipindi
kirefu walipokuwa pamoja. Alionesha wasiwasi kipindi akiwa na mpira,
aliwaonesha washambuliaji wa Simba njia za kupita, na wala hakuwapa
wakati mgumu. Anatakiwa kutazama tena marudio ya dakika 135 ambazo
akiwa na Yondan wameruhusu mabao matano dhidi ya Simba. Ajifunze namna beki tano anavyotakiwa kucheza kutoka kwa Musoti ambaye alicheza vizuri katika mchezo wake wa kwanza tu akicheza na Owino.

MKASA WA BOSI
Wakati timu ikiwa nyuma kwa mabao 3-0, na muda ukizidi kuyoyoma,
mwenyekiti wa klabu ya Yanga, Yusuph Manji akaamua kuondoka zake
uwanjani, baadae wakafuata kina ' Mr. Kazi Nyingi', nao wakaondoka.
Ilikuwa ni ishara ya kushindwa kwa mara ya tatu mfululizo kuwafunga
walivyotarajia mahasimu wao ambao wamemaliza mchezo wa tatu wakienda kucheza na Yanga wakiwa katika ' umbo baya'. Tangu kuahirishwa kwa mchezo huo, ambao tarehe ya awali ilikuwa 14, Simba walijihimarisha zaidi kiuchezaji, na Yanga wakawa wanafanya usajili na kutegemea kushinda. Hali ilikuwa tofauti na matarajio yao, kocha analazimishwa kuwapanga baadhi ya wachezaji, huku akiwa hovyo kudai mahitaji mahitaji muhimu ya timu.
BRANDTS...
Inasemekana aliwaambia wazi kamati ya usajili kuwa wanamleta Kaseja, ila hakuwa ni chaguo sahihi kwa kuwa tayari alikuwa nao, Ally Mustapha na Deogratius Munish ' Dida', pia akawaambia wanamletea Okwi, ila hajui ni wapi atamchezesha zaidi ya kuvuruga mipango yake. Sasa, yupo hatarini kuondoka. Ushindi wa mechi moja, sare mbili na kufungwa moja dhidi ya Simba unamuondoa Yanga?
 HUYU DOGO, SINGANO, POLENI, LUHENDE NA YONDAN

David Luhende alipangwa sehemu ya ulinzi wa kushoto kwa upande wa
Yanga, na Singano akapangwa upande wa kulia kama kiungo mshambuliaji
wa Simba. Mchezo ulikuwa hapa, Luhende mzito, Singano mwepesi, Luhende hanyumbuliki, Singano ananyumbulika, Luhende hana kasi, Singano ana kasi, Luhende hakuwa mjanja, Singano akawa mjanja kama Sungura. Akamshindwa ' dogo', mara akaongezeka, Kelvin. Pamoja na umwamba wake, alimkoma dogo huyu, Kelvin anakwenda spidi, Singano akawa anafanya mbinu zake, mara chenga, anaanza kuunga tera, utamkuta Singano?. Akaona mvute jezi tu, kuliko fedheha kama ya kipindi kile kutoka kwa Ngassa. Poleni, Luhende n Yondan, mlikutana na ' fotokopi' ya Leonel Messi. Nani alikuwa mchezaji bora wa mechi kati ya Singano aliyetumia dakika zisizozidi 70, na Mkude aliyecheza dakika zote 90?. Mchezaji bora ni Logarusic.


0714 08 43 08
 Ndugu na Marafiki wa  Miss tanzania 2013 waliomsindikaza Happiness Watimanywa  Alipotembelea kituo cha watoto yatima cha mjini Morogoro..

JAMES KISAKA AFARIKI DUNIA, MUNGU AILAZE ROHO YA MAREHEMU MAHALA PEMA PEPONI AMINA.

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limepokea kwa masikitiko kifo cha aliyekuwa kocha wa makipa wa Simba, James Kisaka (57) kilichotokea leo asubuhi (Desemba 25 mwaka huu) katika Hospitali ya Burhani, Dar es Salaam.
Msiba huo ni mkubwa katika familia ya mpira wa miguu kwani Kisaka kabla ya kuwa kocha alikuwa mchezaji katika nafasi ya kipa. Mbali ya Simba, timu nyingine alizowahi kudakia ni Ndovu ya Arusha, Volcano ya Kenya na Small Simba ya Zanzibar.
Akiwa mwanafunzi Shule ya Sekondari Tambaza jijini Dar es Salaam aliwahi kuchezea timu za Oysterbay Stars, Eleven Stars ya Msasani, Sigara wakati ikicheza Ligi ya Temeke na Nyota Nyekundu kabla ya kutua Simba.
Pia alikuwemo kwenye timu ya Taifa ya vijana iliyokwenda Zimbabwe kwenye sherehe za uhuru wan chi hiyo mwaka 1980. Vilevile alikuwa mmoja wa wachezaji waliounda kombaini ya Tanzania ya UMISSETA akiwa na akina Said George, Nico Njohole, George Kulagwa na wengine. Hivyo mchango wake katika mchezo huu tutaukumbuka daima.
Kwa mujibu wa kaka wa marehemu, Benny Kisaka, James alikuwa akisumbuliwa na ugonjwa wa miguu kufa ganzi na matatizo ya kutoona vizuri.
Msiba uko nyumbani kwake Mbezi Mwisho (Kwa Yusuf), na anatarajia kuzikwa nyumbani kwao Kijiji cha Lusanga, Muheza mkoani Tanga.
TFF tunatoa pole kwa familia ya marehemu Kisaka, klabu ya Simba na Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) na kuwataka kuwa na subira na uvumilivu katika kipindi hiki kigumu cha msiba huo mzito.
Marehemu Kisaka ameacha mjane na watoto wanne. Bwana alitoa, Bwana ametwaa. Jina lake lihimidiwe.
Boniface Wambura Mgoyo
Kaimu Katibu Mkuu
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)

Tuesday, December 24, 2013

MOHAMED MATUMLA NASIBU RAMADHANI KUMARIZA UBISHA CHRXMAS


Bondia Mohamed Matumla kushoto na Nassibu Ramadhani wakitunishiana misuli baada ya kupima uzito kwa ajili ya mpambano wao leo katika

ukumbi wa friends corner hotel manzese Dar es salaam leo katikati ni promota wa mpambano huo kaike siraju Picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com


Promota kaike Siraju akiwainua juu mikono Bondia Mohamed Matumla kushoto na Nassibu Ramadhani kwa ajili ya mpambano wao wa kugombea pikipiki siku ya sikukuu ya Xmasi Picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com

MTAWALA NA MWESIGA WAPATA MASHAVU TFF.




DAUDA TV: KAMA HUKUBAHATIKA KUYAONA MABAO YA MCHEZO WA SIMBA NA YANGA ( NANI MTANI JEMBE ) HAYA HAPA!

MWAKALEBELA AKANUSHA KUKOSA KIBARUA CHA UKATIBU MKUU TFF - ASISITIZA YUPO TAYARI KUFANYA KAZI NYNGINE NA TFF SIO UKATIBU


MCHEZAJI WA BORA WA LIGI YA BRAZIL - EVERTON RIBEIRO ASEMA ATAICHAGUA MAN UNITED MBELE YA REAL MADRID

Kiungo wa kibrazil Everton Ribeiro kwa mara nyingine ameelezea matamanio ya kujiunga na klabu ya Manchester United. 

United iliwatuma maskauti wake wa vipaji kwenda nchini Brazil kumuangalia staa huyo wa timu ya Cruzeiro na kocha David Moyes anafikiria kutuma ofa rasmi ya £12million ili kukamilisha usajili wa kiungo huyo, ambaye mwezi uliopita alishinda tuzo ya kuwa mwanasoka bora wa ligi ya Brazil.

Hata hiyo, United watakabiliana na upinzani kutka kwa Liverpool na Real Madrid ambao nao wamevutiwa na mchezaji huyo.

Ribeiro ambaye huko nyuma aliwahi kucheza katika mashindano ya vijana na United alipoulizwa na Globoesporte kama angependelea kujiunga na United badala ya Madrid, kiungo huyo mwenye miaka 24 alisema: ‘Ndio, ningependea kucheza United, mfumo ambao United wanaendesha timu ni bora kabisa duniani. Nimewahi kuwepo mahala pale na pia nilienda kupata mafunzo kutoka Alex Ferguson nilipokuwa kinda. ’

Wakala wa mchezaji huyo Robson Ferreira hivi karibuni alinukuliwa akisema: Manchester United wanamtaka Ribeiro,  David Moyes amevutiwa sana. Nilishaenda England na nikaongea rasmi na United.’

FALCAO: RONALDO NI MCHEZAJI BORA ZAIDI YA LIONEL MESSI

Mshambuliaji wa Monaco  Radamel Falcao anaamini kwamba mshambuliaji wa Real Madrid  Cristiano Ronaldo ni mchezaji mzuri kuliko staa wa klabu ya Barcelona Lionel Messi.

Mchezaji huyo wa Colombia anawakubali wachezaji wote wawili, ingawa Falcao anaamini Cristiano ni bora zaidi ya Messi.

"Messi na Cristiano ni wachezaji muhimu na wakubwa duniani leo hii lakini, kwangu mimi naamini Ronaldo ni bora zaidi," alisema mchezaji huyo mwenye miaka 27 alipoongea na El Tiempo.

Falcao pia amesema ni Cristiano Ronaldo anayestahili kuwa mchezaji bora wa dunia katika tuzo za Ballon D'or zitakazotolewa mwezi ujao ambapo Ronaldo anapambana na Ribery pamoja na Messi.

EDIBILY LUNYAMILA APATA NAFUU,

Hali ya winga wa zamani Edibily Lunyamila inaendelea vizuri,leo hii asubuhi mwandishi amepita kwenye hospitali ya Mwananyamala na kukuta Jopo la madaktari saba akiwemo Daktari bingwa wa tiba za michezo,Dr Mwankemwa wakimshughulikia vizuri mgonjwa huyo.

Pia leo asubuhi wachezaji kadhaa wa zamani kama vile Silvatus Ibrahim,Mohamed Hussein na Vincet Peter walipita kumjulia hali mwenzao,Hapo jana uongozi wa Klabu ya YANGA ulifika hospitalini pale ukiongozwa na Mwenyekiti wa kamati ya mashindano Abdallah Bin Kleb,Nahodha wa zamani Ally Mayai na walipanga asubuhi ya leo wamwamishie kwenye hospitali ya Muhimbili,aliyepewa jukumu hilo alikuwa ni mjumbe wa kamati ya utendaji ndugu Mohammed Binda.

'' Jana viongozi wa Yanga tulikubaliana leo tumwamishie hospitali ya Muhimbili lakini tulipofika leo asubuhi madaktari wa hospitali ya Mwananyamala walitusihi tumwache kwanza kwani walikuwa tayari wanamshughulikia,kutokana na huduma nzuri aliyokuwa anapewa na madaktari wa hapa tumeonelea tumwache kwanza'' alinukuliwa Binda akielezea hali ya mgonjwa.


KATIBU MKUU WA SIMBA AACHIA NGAZI AULA TFF - MWESIGA WA YANGA NAE KUMRITHI ANGETILE


KAMATI ya Utendaji ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) imekutana wikiendi iliyopita na kufikia uamuzi wa kuwapa ajira aliyekuwa katibu wa Yanga, Selestine Mwesigwa na wa Simba, Evodius Mtawala.

Mwesigwa atafanya kazi hiyo chini ya uangalizi kwa kipindi cha miezi sita na endapo TFF atamudu nafasi hiyo atapewa muda zaidi, lakini kama atashindwa basi ajira yake itasitishwa mara moja.

Wakati Mwesigwa akiinasa ajira hiyo aliyoshindania vikali na Michael Wambura, mwenzake wa Simba, Mtawala ameula kwenye Mkurugenzi wa Sheria na Masuala ya Utawala ambayo ni nafasi mpya katika shirikisho hilo.

Kufuatia uteuzi huo ni wazi Mtawala atalazimika kuachia ngazi katika nafasi yake ya ukatibu kwenye klabu ya Simba, huku taarifa zilizoifikia Mwanaspoti usiku wa jana Jumatatu, Mtawala ameihakikishia TFF kwamba tayari ameshawasilisha barua yake ya kuacha kazi kwenye klabu ya Simba.

Mwesigwa na Mtawala watatangwa rasmi leo Jumanne na Rais wa TFF, Jamal Malinzi.

DAUDA TV: EXCLUSIVE INTERVIEW YA MH ZITTO KABWE JUU YA MUSTAKABALI WA SOKA LA BONGO.

Monday, December 23, 2013

HII NDIO TAARIFA RASMI YA KUFUKUZWA KOCHA WA YANGA ERNST BRANDTS



Uongozi wa klabu ya Young Africans SC umempatia taarifa (Notice) ya siku ya thelathini (30) kocha mkuu mholanzi Ernie Brandts juu ya kusitisha mkataba wake kuanzia jana Disemba 22 mwaka huu.
Maamuzi hayo yanafuatia muenendo wa matokeo mabaya katika michezo iliyopita ya Ligi Kuu, kirafiki na bonanza la Nani Mtani Jembe dhidi ya Simba SC mwishoni mwa wiki.
Hatua ya Young Africans SC kusitisha huduma na Brandts isichukuliwe kama chuki bali ni moja ya sehemu ya kuhakikisha tunaboresha benchi la ufundi ili tuweze kupata matokeo mazuri katika Mashindano yanayotukabili.
Ukitazama uwezo wa mchezaji mmoja mmoja wa Yanga SC na wapinzani wetu, na soka tulilocheza kwenye mchezo wa mwishoni mwa wiki kwa kweli ni dhahiri mwalimu amefikia mwisho kimbinu na hana njia mbadala.
Young Africans SC imekua ikicheza chini ya kiwango katika michezo ya Ligi Kuu hali iliyoplekea kupata ushindi kwa tabu na wakati mwingine timu kupoteza pointi.
Kufuatia kupewa taarifa ya siku 30, Brandts ataamua mwenyewe kama ataendelea kusimamia mazoezi ya timu au kuondoka moja kwa moja kabla ya muda huo ukiwa haujakamilika.
Ikiwa Brandts ataondoka mapema timu itaendelea na mazoezi kama kawaida katika kila siku asubuhi katika uwanja wa bora kijitonyama kujiandaa na mzunguko wa pili wa Ligi Kuu na mashindano ya kimataifa chini ya kocha msaidizi Fred Felix “Minziro”.
Ili kuhakikisha timu inafanya vizuri katika mzunguko wa pili wa Ligi Kuu ya Vodacom na mashindano ya kimataifa uongozi unakamilisha maandalizi ya safari ya kambi nje ya nchi na taratibu zote zitakapokamilika tutawajulisha.
Aidha uongozi upo katika mchakato wa kumapata mrithi wa Brandts ambaye ataungana na timu kwa ajili ya maandalizi ya mzunguko wa pili na Mashindano ya klabu Bingwa Afrika.
Mwisho tunawaomba wanachama, wapenzi na washabiki wa Yanga wasivunjike moyo kufuatia matokeo ya bonanza mwishoni mwa wiki, uongozi unajipanga kuhakikisha timu inaimarika kwenye benchi la ufundi na kurudisha furaha katika mzunguko wa pili wa VPL.


Abdallah Bin Kleb
Mwenyekiti - Kamati ya Mashindano
Young Africans Sports Club.



DAR ES SALAAM
23 Disemba, 2013

BREAKING NEWS…..! HALI NI MBAYA…! LUNYAMILA ANAPUMULIA MASHINE HOSPITALI YA MWANANYAMALA.


WINGA wa zamani wa Yanga na Taifa Stars, Edibily Lunyamila leo hii asubuhi amekimbizwa katika hospitali ya Mwananyamala baada ya kusumbuliwa na kifua na sasa anapumua kwa msaada wa mashine.

Mtandao huu ulifanikiwa kufika hospitalini hapo muda mfupi baada ya winga huyo kukimbizwa hospitalini hapo baada ya kuzidiwa tangu jana usiku akiwa nyumbani kwake Mbezi jijini Dar es Salaam.

Shaffihdauda.com imemshuhudia Lunyamila akiwa amelala kitandani katika wodi ya wanaume namba namba 5 kitanda namba 16 katika hospitali hiyo ya rufaa ya Kinondoni.





Daktari Madirisha Pascal anayemuhudumia winga huyo wa zamani, Lunyamila anasumbuliwa na tatizo la kifua ambalo linamfanya ashindwe kupumua vizuri.

“Kama mnavyomuona anapumua kwa msaada wa mashine na bado tunaendelea kumfanyia uchunguzi ili kubaini nini kinachomsumbua zaidi,” alisema Pascal.

Mmoja wa ndugu wa Lunyamila, Lameck John alisema kwamba, mchezaji huyo wa zamani alianza kujisikia vibaya jana Jumapili na leo asubuhi hali yake ilibadilika ndipo walipomkimbiza hospitali.




 Lunyamila alivyokuwa enzi anaichezea Yanga..



 

“Alianza kulalamika hawezi kupumua na kifua kinamsumbua pia mbavu zilikuwa zikimuuma, baada ya majibu ya vipimo tutajua kinachomsumbua zaidi,” alisema Lameck.

Kutokana na hali iliyoonekana hospitalini hapo, Lunyamila anahitaji huduma ya haraka ili kuweza kuokoa uhai wake kwani anapumulia mashine akiwa katika sehemu yenye joto kali hivyo anapambana na vitu vingi kwa wakati mmoja...

Taarifa za kiuchunguzi zilizofanywa na mwandishi wetu zimebaini Lunyamila anasumbuliwa na ugonjwa wa moyo.
''Nilikuja jana hospitali ya mwananyaala ikagundulika moyo wangu umekuwa mkubwa,hivi sasa naenda muhimbili kwa ajili ya vipimo zaidi nikifika na kukutana na daktari nitakujulisha ''
ilipofika mchana wa leo mwandishi alipokea simu kutoka kwa Lunyamila akimwambia ameambiwa arejee tena hospitali ya Mwananyamala.

KASEBA AMCHAKAZA ALIBABA KWA K,O RAUNDI YA 4


Bondia Japhert Kaseba kushoto akioneshana umwamba wa kutupiana makonde na Alibaba Ramadhani wakati wa kugombania ubingwa wa Taifa uliofanyika Manzese Dar es salaam Kaseba alishinda kwa KO ya raundi ya nne ya mpambano huo Picha na superdboxingcoach.blogspot.com
Kanda kabongo akimuhuumia Japhert Kaseba
Bondia Omari Nampekecha 'peche boy' kushoto akipambana na hasani Kiware wakati wa mpambano huo nampekecha alishinda kwa pointi picha na superdboxingcoach.blogspot.com
Kaseba akiwa na familia yake pamoja na mashabiki baada ya kushinda mchezo wake
Bondia Pendo Njau kushoto akiwa na bondia Llulu Kayage wakati wa mpambano huo
mashabiki wakiangalia mpambano
Wapiganaji wa mpambano wa Kick Boxing kareem kutch kushoto akipambana na Hassani Juma 'Tata Boy' wakati wa mpambano huo kutch alishinda kwa point picha n
Wapiganaji wa mpambano wa Kick Boxing kareem kutch kushoto akipambana na Hassani Juma 'Tata Boy' wakati wa mpambano huo kutch alishinda kwa point picha na


Written by

0 maoni: